Mseminari Mtanzania wa Parokia ya Kigoma atekwa nyara Nigeria

 

Mseminari wa Kanisa Katoliki, Dominiki Melkiori Mahinini, mzaliwa wa Parokia ya Kabanga katika Jimbo la Kigoma, ametekwa nyara na watu wasiojulikana nchini Nigeria, akiwa na Padre Paul Sanoga raia wa Burkina Faso.

Kwa mujibu wa barua ya Askofu wa Jimbo Katoliki Kigoma Joseph Mlola, viongozi hao wa Kanisa walitekwa nyara na kundi la watu wasiojulikana mapema usiku wa kuamkia tarehe 03/08/2023 katika Parokia Mt. Luka Gyenda Jimbo la Minna, nchini Nigeria.

Askofu Mlola ameeeleza katika barua yake hiyo aliyoiandika jana tarehe 04/08/2023, kwamba Mseminari Dominiki Melkiori Mahinini alikuwa Nigeria katika mwaka wake wa uchungaji kabla ya kuanza masomo yake ya Teolojia.

Kufuatia tukio hilo Kanisa Katoliki Jimbo la Kigoma kwa kushirikiana na Mapadre Wamisionari wa Afrika (White Fathers), Askofu Mlola anawaalika mapadre wote, watawa wote, Waumini Jimbo la Kigomana watu wote wenye mapenzi mema kusali kuwaombea watumishi hao waliotekwa.



Chapisha Maoni

0 Maoni