Rais wa FIFA Gianni Infantino amesema mafanikio ya Kombe la
Dunia la Wanawake yamewazima kidomodomo wakosoaji wa uamuzi wa kuongeza ushiriki wa mataifa
32 kwenye michuano hiyo.
Kulikuwa na wanaohoji kuongezeka timu kutoka 24, kuwa kungepelekea
timu za upande mmoja kutawala katika michuano hiyo iliyofanyika Australia na New
Zealand.
Hata hivyo, Nigeria, Afrika Kusini, Jamaica na Morocco,
ambazo hazipo katika nafasi 40 ya ubora wa soka duniani, zilifanikiwa kuvuka hatua
ya makundi.
0 Maoni