NMB yamwaga msaada wa madawati kwa shule za msingi Ilala

 

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amekabidhiwa msaada wenye thamani zaidi ya milioni 51 katika shule ya Msingi Mtakuja Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha sekta ya Elimu.

RC Chalamila amekabidhiwa madawati 200 kwa ajili ya Shule ya Msingi Mtakuja, Miembeni, Kombo na vingunguti, Bati 400 shule ya msingi Airwing na Sekondari karezange, Meza na viti vyake 100 kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Kivule na Gerezani pia meza na viti 34 kwa ajili ya walimu wa shule ya msingi Bonyokwa,

RC Chalamila ameipongeza na kuishukuru Benki ya NMB kwa msaada huo na kutoa rai kwa wadau wengine kuendelea kusaidia maboresho katika Sekta ya elimu katika Mkoa huo

Hata hivyo Mhe Albert Chalamila amepokea Changamoto zingine zilizowasilishwa kwake na wanafunzi wa shule ya msingi Mtakuja ikiwemo ubovu wa miundombinu na matundu ya vyoo ambapo ameutaka uongozi wa Jiji la Dar es Salaam kutatua Changamoto hiyo mara moja.

Aidha Meneja wa Benki ya NMB kanda ya Dar es Salaam Bwana Dismas Prosper akikabidhi msaada huo amesema msingi mzuri wa jamii unajengwa kupitia upatikanaji wa elimu bora kama mdau mkubwa wa sekta ya elimu nchini tunaunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita katika upatikanaji wa elimu bora katika kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia.

Kwa Upande wa Mkuu wa Wilaya Mhe Edward Mpogolo ameishukuru Benki ya NMB kwa msaada huo ambao unalenga kuboresha sekta ya elimu katika Wilaya ya Ilala, vilevile amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kutekeleza maelekezo na maagizo yake kwa wakati.

Chapisha Maoni

0 Maoni