Mwanamke raia wa Canada amefungwa jela miaka 22 nchini
Marekani kwa kosa la kutuma barua zenye sumu ya ricin, ikiwamo kwa Donald Trump
wakati akiwa rais.
Mwanmake huyo Pascale Ferrier, 56, alikubaliana na hukumu
hiyo Januari 2020, baada ya kukiri mahakamani makosa ya kutumia silaha za
kibailojia.
Barua hiyo hatari iliyotumwa kwa Trump, iligundulika kabla
ya kufika Ikulu ya Marekani (White House) Septemba 2020.
Mwana mama huyo Ferrier aliiambia Mahakama kwamba anajuta kuwa
mpango wake huo ulishindwa na hakuweza kumdhuru Trump.
0 Maoni