Timu ya wataalamu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imetembelea
kampuni ya PLASCO Tanzania, ambayo ipo mbioni kutoa msaada wa tanki la maji
lenye ujazo wa lita laki mbili.
Tanki hilo linathamani ya shilingi milioni 150, litasaidia
katika kutatua changomoto ya ukosefu wa maji ambayo huwa inaikabili hospitali hiyo
ya taifa hasa wakati wa kipindi cha kiangazi.
Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa MNH Mhandisi Jonas Bayona
amesema lengo la ziara hiyo ni kujionea teknolojia mpya ya utengenezaji
matanki, kujifunza namna ya kutumia na kurekebisha pale inapotokea changamo
yoyote.
0 Maoni