Mwenyekiti wa zamani wa Simba SC Ayoub Chamshama amefariki
dunia nchini India alipokuwa amepelekwa kupatiwa matibabu.
Taarifa ya kifo hicho imetolewa na mtoto wake Soud Ayubu
Chamshama wa Chang'ombe Dar es Salaam.
Taarifa hiyo imesema kifo cha Chamshana kimetokea tarehe 11
Agosti 2023 nchini India alipokuwa kwa matibabu.
Mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumanne tarehe 15
Agosti 2023 kijijini kwao Kilole, Lushoto, Mkoani TANGA.
Enzi za uhai wake marehemu Chamshama alishika nyadhifa
mbalimbali. Alikuwa Meneja Mkuu wa kampuni ya Tanzania Tea Blenders, vilevile
alihudumu kwa muda mrefu kama Mwenyekiti wa klabu ya Simba SC na pia alikuwa
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Temeke.
0 Maoni