Mgombea urais Ecuador apigwa risasi na kufa kwenye kampeni

 

Mgombea urais nchini Ecuador katika uchaguzi ujao aliyekuwa akipiga kampeni ya kupiga vita rushwa na magenge ya uhalifu, amepigwa risasi na kufa akiwa kwenye mkutano wa kampeni.

Mgombea huyo Fernando Villavicencio, ambaye ni mbunge wa bunge la nchi hiyo, alishambuliwa kwa risasi wakati akiondoka kwenye mkutano wa hadhara Jijini Quito, Jumatano.

Mgombea huyo ni mmoja kati ya waliotoa madai ya kuwapo kwa uhusiano baina ya makundi yanayoratibu uhalifu na maafisa wa serikali ya Ecuador.

Genge la uhalifu la Los Bobos ama Mbweha lenye wafuasi 8,000 nchini humo, ambao wengi wao wanatumikia vifungo magerezani limedai kuhusika na shambulizi hilo.

CHANZO: BBC

Chapisha Maoni

0 Maoni