Lionel Messi amepongezwa kama mchezaji bora duniani wakati
akifunga goli lake la 10 katika michezo saba na kuisaidia Inter Miami kutwaa
kombe la kwanza.
Raia huyo wa Argentinian alifunga goli kwenye kona ya juu ya
goli kwa shuti la nje ya boksi na kuipatia Miami goli la kuongoza dhidi ya Nashville
SC katika fainali ya kombe la ligi.
Fafa Picault alisawazisha goli hilo na mchezo ukaenda kwenye
mikwaju ya penati, ambapo Inter Miami iliipuka na ushindi wa magoli 10-9.
0 Maoni