Watu watatu wamekamatwa, baada ya wafanyakazi wa kampuni ya kutengeneza jibini ya Kenya kudai wamelazimishwa kuvua nguo ili kumbaini ni nani yupo kwenye
siku zake za hedhi.
Meneja wa Kampuni hiyo ya Brown’s Food Company, aliwakusanya wafanyakazi
wanawake ili kubaini ni nani alitupa pedi katika pipa lisilosahihi, afisa mmoja
amesema.
Meneja huyo aliwaagiza wafanyakazi wanawake kuvua nguo, baada
ya jitihada zake za kumpata mwanamke aliyetupa pedi hiyo kimakosa kushindwa kuzaa
matunda.
Kampuni ya Brown's imesema kwamba imemsimamisha kazi meneja
wake huyo anayetuhumiwa kufanya udhalilishaji huo wa kijinsia, ili kupisha
uchunguzi.
CHANZO: BBC
0 Maoni