Washirika wa Marekani wapinga kutumika mabomu ya cluster

 

Washirika kadhaa wa Marekani, wameonyesha kutoafikiana na uamuzi wa nchi hiyo kuipatia Ukraine mabomu ya aina ya cluster.

Ijumaa, Marekani ilithibitisha imepeleka silaha hiyo yenye utata nchini Ukraine, huku Rais Joe Biden akiita hatua hiyo kuwa ni “uamuzi mgumu mno”.

Kwa upande wa Uingereza, Canada, New Zealand na Hispania wamepinga matumizi ya silaha hiyo.

Mabomu ya cluster yamepigwa marufuku katika zaidi ya nchi 100 kutokana na hatari kwa raia  inayosababishwa na mabomu hayo.

Mabomu hayo yanaporushwa husambaza mabomu madogo mithili ya risasi yenye kuua hata watu wasio na hatia.

Chapisha Maoni

0 Maoni