Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) chini ya Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mkuu wa Majeshi (Mstaafu) Jenerali George Waitara leo Februari 05, 2026 inaendelea na kikao cha 213 Jijini Dodoma. Kikao hicho kinajadili masuala mbalimbali yanayohusu Uhifadhi, Utalii na Uwekezaji.
Vikao hivyo vimeanza leo vikitanguliwa na kikao cha Kamati ya Himasheria na Usimamizi wa Hifadhi inayoongozwa na Mwenyekiti wake Dkt. Robert Fyumagwa na kikao cha Kamati ya Utalii na Huduma za Shirika kilichoongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Bw. Athumani Kwariko.



0 Maoni