Manchester United wanamatumaini ya kukamilisha dili la
kumnasa kipa wa Inter Milan Andre Onana.
Kocha Erik ten Hag yupo makini katika kutatua tatizo la
nafasi ya kipa Old Trafford, kutokana na uwezekano wa kumkosa kipa wao David de
Gea.
Mkataba wa De Gea kukaa Old Trafford ulimalizika mwishoni mwa
mwezi uliopita na bado hajapewa ofa ya kuongezewa mkataba mpya.
Onana, mwenye umri wa miaka 27 hajafungwa goli kwenye mechi nane
kati michezo 24 ya ligi ya Italia ya Seria A aliyocheza msimu huu.
0 Maoni