Kundi la watalii wa ndani wapatao 21, wametumia kikamilifu
ofa maalum ya Sabasaba kwenda kutalii katika Hifadhi ya Magofu ya kale Kilwa
Kisiwani iliyo chini ya Usimamizi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori
Tanzania (TAWA).
Ofa hii imelenga kuhamasisha Utalii wa ndani na kuwawezesha
watanzania wote kutembelea hifadhi hiyo Kwa kupunguzo kubwa la gharama ambapo
mtalii Kwa kulipia gharama ya Shillingi 130,000/= ataweza kutalii baharini katika visiwa vya Kilwa Kisiwani na
Songo Mnara Kwa kutumia boti la Kisasa lenye kioo maalum chenye kumwezesha
mtalii kuona mandhari na viumbe mbalimbali vilivyopo chini ya bahari Kwa siku
mbili
Kupitia malipo ya kiasi hicho mtalii pia ataweza kupata chakula, vinywaji na viburudisho mbalimbali
Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA)
inaendelea kuwahamasisha watanzania wote kutumia kipindi hiki cha maonesho ya
Sabasaba kutembelea hifadhi zake zote nchini hususan Kilwa Kisiwani na Songo
Mnara kwani ni kipindi maalum chenye punguzo maalum Kwa watalii wa ndani
Na. Beatus Maganja
0 Maoni