Maandamano yakuipinga serikali ya Kenya yamekuwa yakiendelea
katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo kupinga kupanda kwa gharama za maisha.
Maaandamano hayo yaliyoitishwa na chama cha Azimio leo yamepelekea
kusita kwa baadhi ya shughuli katika maeneo mbalimbali za nchi hiyo.
Huko Nakuru polisi wamekuwa wakipambana na waandamanaji ambao
wamechoma moto matairi barabarani na kuweka mawe.
Katika eneo la Mathare, Jijini Nairobi waandamanaji wamekuwa
wakiwatupia mawe polisi wanaojaribu kuzima maandamano yao.
Waandamanaji wa huko Nyamira wao wamekuja na aina yao ya maandamano
kwa kubeba sufuria tupu katika kuonyesha hawana chakula.
Nako Mombasa polisi wa usalama barabrani wamelazimika kukaa
kando kupisha askari wa kudhibiti fujo kukabiliana na waandamanaji.
Chanzo: Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii Kenya
0 Maoni