Watu sita, wakiwamo watoto watatu wameuawa kwa kuchomwa na
kisu leo asubuhi kwenye shule ya Chekechea katika mkoa wa kusini mwa China wa
Guangdong.
Polisi wamesema kwamba wamemkamata kijana wa kiume mwenye
umri wa miaka 25, ambaye jina lake la ukoo ni Wu kwenye mji wa Lianjiang.
Wengine waliouwa katika tukio hilo ni mwalimu na wazazi
wawili, shirika la habari la AFP, limevinukuu vyombo vya habari vya China. Mtu
mmoja pia amejeruhiwa.
0 Maoni