Boti yenye wahamiaji 200 wa Afrika yatoweka majini

 

Waokoaji wa Hispania wanatafuta boti lililotoweka likiwa na wahamiaji 200 wa Afrika, ambao wametoweka kwa zaidi ya wiki kwenye eneo la kisiwa cha Canary.

Waokoaji hao wa kundi la Walking Borders, wamesema boti hiyo ilikuwa inatokea Kafountine, mji wa pwani ya kusini mwa Senegal umbali wa kilomita 1,700, kutoka Tenerife.

Kundi hilo limesema kwamba watoto wengi walikuwamo kwenye boti hiyo, ambapo pia boti nyingine mbili za wahamiaji wa Afrika zimeripotiwa nazo kutoweka majini.

Chapisha Maoni

0 Maoni