Mwanafunzi wa kike aghushi nakala ya matokeo ya kitaifa

 

Mwanafunzi wa kike mwenye umri wa miaka 19, aliyeibua utata iwapo alipata alama za juu za ufaulu kwenye mtiahani wa taifa, amekiri kuwa alighushi matokeo ya mtihani wa taifa wa mwaka huu.

Mgogoro wa matokeo ya mwanafunzi huyo Ejikeme Joy Mmesoma ulitinga kwenye Bunge la Nigeria, ambapo wabunge walilazimika kujadili suala la matokeo ya mwanafunzi huyo.

Ejikeme Joy Mmesoma amejikuta akipongezwa tangu alipojitokeza na kutangaza amepata ufaulu wa alama 362 katika mtihani wa taifa na kuongoza nchi nzima.

Alichofanya mwanafunzi Ejikeme Joy Mmeni ni kujiposti kwenye mtandao akiwa na nakala ya matokeo ya kughushi akithibitisha kuwa yeye ndiye mwanafunzi bora kitaifa.

Mmoja wa wafanyabiashara nchini humo aliiona posti hiyo na kuvutiwa na matokeo hayo mazuri ambapo aliahidi kumfadhili masomo yake kwa gharama sawa na dola 4,000 za Marekani.

Chapisha Maoni

0 Maoni