Maduka makubwa ya bidhaa ya Uingereza yameaza kuweka alama
za usalama kwenye mapande ya nyama na jibini katika kukabiliana na wimbi la wizi
unaofanywa na wateja wasio waaminifu.
Baadhi ya maduka yamechukua hatua zaidi ya kuweka idadi
chache ya bidhaa hizo kwenye mashubaka, katika jitihada za kupunguza wizi.
Hii inafuatia kutolewa kwa takwimu na shirika la BBC,
zinazoonyesha kwamba sasa wizi wa bidhaa madukani umekuwa ni janga, kutokana na
kupanda kwa gharama za maisha.
Wamiliki wa maduka ya bidhaa wamesema kwamba wamelazimika
kutumia fedha nyingi katika kuimarisha ulinzi.
Mwezi Machi, vikosi vya polisi vay England, Wales na
Kaskazini Ireland walitoa rekodi ya matukio 33,000 ya vibaka waliiba bidhaa madukani.
0 Maoni