Pence kujitosa kuwania urais na Trump kwa tiketi ya Republican

 

Mbio za kuwania urais wa Marekani 2024, kwa tiketi ya chama cha Republican zinakaribia kupanda joto, kufuatia vigogo wawili zaidi kutarajiwa kuingia kwenye kinyang’anyiro.

Aliyekuwa Makamu wa Rais Mike Pence na aliyekuwa Gavana na News Jersey Chris Christie wanajiandaa wiki ijayo kuingia ulingoni.

Wagombea hao wanatarajia kutoa upinzani wa aina yake kwa kwa aliyekuwa rais wa Marekani Donald Trump.

Hatimaye mshindi wa upande wa Republican anatarajiwa kuchuana na Rais Joe Biden, wa Democrat, katika uchaguzi wa Novemba mwakani.

Chapisha Maoni

0 Maoni