Mchezaji wa Yanga aliyekataa kuichezea klabu hiyo Feisal
Salum maarufu kama Fei Toto ameendelea kutema nyongo, huku akiwatuhumu baadhi
ya viongozi wa klabu hiyo kuwa walimsingizia kuwa yeye anauza mechi.
Fei Toto amesema kuwa yeye anawapenda mashabiki wa Yanga,
ila hawaambiwi ukweli kuhusiana na nini haswa kilichomtoa klabu hiyo ya Yanga
aliyoichezea tangu aingie mkataba wa kwanza mnamo mwaka 2018.
“Mashabiki wa Yanga mimi nawapenda ila hawajui kilichonitoa
Yanga, nimeondoka Yanga kwa ajili ya manyanyaso,” alisema Fei Toto wakati
akihojiwa kwenye kipindi cha Power Breakfast cha Clouds FM na kuongeza, ”Mimi
niliambiwa na baadhi ya viongozi kuwa ninauza mechi”.
Akiongea kwa huzuni Fei Toto alisema aliambiwa na mtu
aliyendani ya kamati ya klabu hiyo kuwa baadhi ya viongozi wanamtuhumu kuwa anauza
mechi, ambapo walimueleza kama hataki kucheza mpira arudi kwao Pemba.
“Nilipoambiwa maneno hayo yaliniuma na ilinibidi niwapigie
simu wahusika lakini hawakunipokelea simu, ila matusi yakawa mengi na
manyanyaso, kunawakati mimi nililia uwanjani lakini watu hawakujua ninalilia
nini,” alisema Fei Toto.
Akifananua kuhusu kauli ya kula ugali na sukari, Fei Toto
alisema kuwa hiyo ilikuwa ni nyakati za nyuma wakati kabla hajaja mfadhili wa
sasa, kwani kunawakati alikuwa anaishi kwa shida bila ya kulipwa mshahara hadi kwa
miezi mitatu.
Hata hivyo, amesema tangu ameingia Yanga amekuwa anapitia mengi,
ila kwa mshahara huu wa sasa umekuwa na manyanyaso mengi, jambo ambalo
limechangia kwa kiasi kikubwa yeye kufikia uamuzi wa kujitoa kwenye klabu hiyo.
“Kuna wakati mama yangu anakuja kuongea na uongozi wanamdhalilisha,
mama alikuja Dar es Salaam wakamkalisha Salamander kuanzia asubuhi hadi jioni,
kisha wakampeleka Avic Town, haitoshi bado wanamtukana, wanamtolea maneneo
mabovu na kejeli,” alisema Fei Toto.
Fei Toto aliyeonyesha kuchukizwa kutukaniwa mama yake
amesema, “Mama yangu ndio msimamizi wanngu halafu anajitokeza mtu kapewa simu
ya macho matatu anawaaminisha wananchi mimi ni mbaya, anamuita mama yangu andazi!?”.
0 Maoni