Maafisa wa Ikulu, akiwamo Rais na Naibu Rais, Mawaziri na
Wabunge, wanatarajiwa kupatiwa nyongeza ya mishahara ya asilimia 14 katika
kipindi cha miaka miwili ijayo, kuanzia mwezi ujao, kufuatia mapendekezo ya
Tume ya Miashahara na Maslahi (SRC) ili kupunguza makali ya kupanda kwa gharama
za maisha.
Iwapo mapendekezo hayo yataridhiwa, maafisa hao watapata
ahueni kubwa kutokana na madhara ya kuendelea kuwapo kwa mfumuko mkubwa wa bei,
ambao umekuwa ukiathiri vipato vyao kutokana na gharama za bidhaa za mahitaji
ya msingi.
CHANZO: Nation
0 Maoni