Mashambulizi ya makombora ya Urusi yamewaua mapacha wakike katika eneo la kati la Kramatorsk mashariki mwa Ukraine kwenye mkoa wa Donetsk.
Mapacha hao
ambao ni miongoni mwa watu kumi waliouawa katika mashambulizi hayo wametajwa
kuwa ni Yuliya na Anna Aksenchenko wenye umri wa miaka 14.
Eneo la Kramatorsk
linamilikiwa na Ukraine, lakini lipo karibu eneo la nchi hiyo linalokaliwa kimabavu na wanajeshi wa Urusi.
0 Maoni