Watoto wa familia moja wafa wakichimba mchanga Muleba

 

Wakazi wa Kijiji cha Magata Kata ya Karutanga mkoani Kagera wamejawa na simanzi baada ya watoto wawili wa familia moja kufa baada ya kufunikwa na kupondwa mawe wakati wakichimba mchanga katika eneo la Marahara.

Diwani wa Karutanga, Alhaji Yakubu Mahamoud, amewataja watoto waliokufa kuwa ni  Samsoni Eliud (13) na Emmanuel Eliud (10) ambao wote walikuwa ni wanafunzi wa Shule ya Msingi Magata.

Diwani Mahamoud amesema kuwa watoto hao  waliokuwa wakilelelewa na mama yao walipotea  Juni 26 mwaka huu na walitafutwa katika maeneo yote hawakuweza kupatikana na Juni 27 watoto hao ndipo walipopatikana wakiwa tayari wamekufa baada ya kufukiwa  na mawe wakati wakichimba mchanga.

Kufuatia tukio hilo Mkuu wa wilaya ya Muleba Dkt. Abel Nyamahanga alifika katika eneo hilo na kupiga marufuku na kuzuia mtu yeyote kufanya shughuli za uchimbaji wa mchanga kwa kuwa eneo hilo sio salama na kuagiza kukaguliwa maeneo yote ya uchimbaji wa mchanga katika wilaya hiyo ili kudhibiti maafa kama hayo kutokea.

CHANZO: Mwandishi wa Kagera 

Chapisha Maoni

0 Maoni