Mwanamke nchini Australia mwenye umri wa miaka 48 ameweza
kuishi siku tano akiwa amekwama msituni kwa kula pipi na kunywa wine chupa moja.
Mwanamke huo Lillian Ip alikuwa kwenye safari fupi
aliyoianza siku ya Jumapili, akisafiri kwenye barabara inayokatiza kwenye msitu
mzito katika jimbo la Victoria.
Lakini kwa bahati mbaya mwanamke huyo akakatiza barabara
yenye kikomo, na gari lake kukwama kwenye matope.
Mwanamke huyo ambaye si mnywaji wa kileo, alikuwa na chupa
ya wine tu kwenye gari ambayo alikuwa ameinunua kwa ajili ya kuitoa kama
zawadi.
Baada ya kukwama kwa siku tano, mwanamke huyo alibainika na
kikosi cha dharura Ijumaa baada ya kumuona wakitumia helkopta.
0 Maoni