Mtu mwenye silaha amewafyatulia risasi na kuwaua watu wanane kwenye duka la bidhaa kaskazini mwa Dallas, watoa huduma wa dharura Texas wamesema.
Mamia ya watu wameondolewa kwenye jengo la duka la Allen
Premium, ambapo mashuhuda wamesema mtu huyo alifyatua risasi hovyo kwa watu
wapitao.
Afisa mmoja wa polisi aliyekuwapo katika eneo la tukio
ameuawa kwa risasi na mtu huyo.
Baadhi ya wahanga wa tukio hilo ni watoto. Watu wapatao saba
wanatibiwa hospitalini, watatu miongoni mwao hali zao ni mbaya.
0 Maoni