Bloga maarufu nchini Uganda Ibrahim Tusubira aka Isma Olaxes
ameuawa kwa kupigwa risasi katika kitongoji cha Kyanja.
Tusubira alifariki papo hapo baada ya gari lake lenye
usajili namba UBK213D kushambuliwa kwa risasi usiku wa jumamosi nje ya geti
la nyumba yake.
Taarifa ya polisi imesema kuwa Tusubira ameuawa wakati
akiendeshwa na dereva wake aliyetambuliwa kwa jina la Wasswa Mathias.
Hivi kribuni Bloga Tusubira ambaye alikuwa ni Mwenyekiti wa Chama
cha Mabloga Uganda alinukuliwa akisema kunawatu wanapanga kumuua.
0 Maoni