Miili zaidi mitano imefukuliwa leo Alhamis, ikiwa ni sehemu
ya uchunguzi katika eneo la dhehebu tata la Mchungaji Paul Mackenzie aliyeagiza
waumini wake wafunge hadi kufa ili wakutane na Yesu.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Rhoda Onyancha, amesema miili
iliyofukuliwa hadi sasa imefikia 150, na kuongeza kuwa leo ndio wamefukua idadi
ndogo ya miili ikilinganishwa na siku za nyuma.
Onyancha ameeleza kuwa wanaume wawili watu wazima
wameokolewa leo, wote hali zao ni nzuri, na kufanya idadi ya waliookolewa
kufikia watu 72.
Ameongeza kuwa idadi ya watu walioripotiwa kupotea
inaendelea kuongezeka na kufikia watu 594 hadi kufikia leo Alhamis na idadi ya
miili iliyochukuliwa kipimo cha DNA imefikia 93.
Waumini wengine 14 kanisa hilo lililopo eneo la Shakahola
nchini Kenya wameunganishwa na familia zao.
0 Maoni