Mahakama imemtia hatiani aliyekuwa rais wa Marekani Donald
Trump kwa kumdhalilisha kijinsia mwandishi wa makala kwenye jengo moja New York
katika miaka ya 1990.
Hata hivyo mahakama haijamtia hatiani Trump kwa kumbaka
mwandishi huyo E Jean Carroll katika chumba cha kubadilishia nguo cha Bergdorf
Goodman.
Mahakama pia imemtia hatiani Trump kwa kukashifu kutokana na
kumtuhumu mwandishi huyo kuwa “tapeli na muongo”.
Hii ni mara ya kwanza kwa Trump kutiwa hatiani kisheria na mahakama
kuhusiana na tuhuma za udhalilishaji kijinsi zinazomuandama.
0 Maoni