Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amemuagiza msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mutungi kuitisha kikao maalumu cha Baraza la vyama vya siasa.
Rais Samia ametoa maagizo hayo leo Mei 6, 2023 Ikulu ya Chamwino Dodoma wakati akiongoza Kikao cha Viongozi mbalimbali wa Serikali kinachohusu kuanza kwa Mchakato wa Katiba mpya.
Katika taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais Ikulu Zuhura Yunus imesema Rais Samia amesisitiza lengo la kuitisha mkutano huo ni kuwashirikisha wadau katika kutathmini utekekelezaji wa mapendekezo ya kikosi kazi kilichokuwa kikiratibu maoni ya watu kuhusu demokrasia ya vyama vingi nchini.
Mbali na mchakato wa katiba mpya masuala mengine yanayotarajiwa ni pamoja na marekebisho ya sheria mbalimbali.
0 Maoni