Prof. Mbarawa aomba trilion 3.5 bajeti Ujenzi, Uchukuzi

 

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa ameliomba Bunge kuidhinisha  jumla ya Shilingi 3,554,783,957,000.00.


Prof. Mbarawa ameyasema hayo amewasilisha mpango wa makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2023/24, kati ya fedha hizo, Shilingi 1,468,238,449,000.00 ni kwa ajili ya Sekta ya Ujenzi na Shilingi 2,086,545,508,000.00 ni kwa ajili ya Sekta ya Uchukuzi.


Mwaka wa fedha 2022/23, Sekta ya Ujenzi ilitengewa jumla ya Shilingi 44,293,050,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Kati ya fedha hizo, Shilingi 40,638,652,000.00 ni kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi wa Wizara na Taasisi zake na Shilingi 3,654,398,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo ya Wizara na Taasisi zake.

Chapisha Maoni

0 Maoni