Nabii mwenye wake 42, biblia ya vitabu 93 kuhojiwa Kenya



Hatua za uchunguzi wa makanisa nchini Kenya zinaendelea na kumuibua Mhubiri Ronald Wanyama, mwenye wake 42 na watoto 289.

Msako huo wenye lengo la kuyabaini makanisa yasiyosajiliwa na yanayotoa mafundisho utata umemkamata katika eneo la Bungoma.


Mhubiri huyo anajulikana kama Nabii Yohana kutoka Kenya, ametakiwa kufika mbele ya Kamanda wa Polisi wa Bungoma, Juni 2, mwaka huu kwa ajili ya kujieleza.



Mhubiri huyo mwenye umri wa miaka 83 anaendesha  kanisa liitwalo Church for All Nations amekuwa na kishindo cha kustaajabisha haswa baada ya madai ya kuzindua biblia yake yenye vitabu 93 na sarafu yake.


Kwa mujibu wa Franci Kooli, Kamanda wa Polisi Kaunti ya Bungoma, amesema mhubiri huyo atahojiwa na kuchunguzwa  kwa madai ya mafundisho yenye utata na  jinsi kanisa lake linavyofanya kazi.


Katika biblia yake  inasemekana kuwa alibuni na kuongeza amri zake mwenyewe, akiongeza amri mbili zaidi katika zile kumi ambazo hujulikana katika dini ya Kikristo.

Chapisha Maoni

0 Maoni