Polisi wamekamata kilo 290 za bangi kwenye ndege iliyosajiliwa kwa jina la tawi la kanisa moja la Kiinjilisti la nchini Brazili.
Ndege hiyo yenye injini moja ilikuwa inajiandaa kuondoka kwenye
hema la kuhifadhia ndege katika uwanja
wa kimataifa wa Belém.
Mtu mmoja amekamatwa katika eneo la tukio, licha ya kujaribu
kutaka kukimbia vyombo vya dola.
Picha zilizotolewa na Polsi wa Shirikisho wa Brazili
zinaonyesha bangi hiyo iliyobainika kwenye ndege hiyo ya kanisa.
0 Maoni