Mwanamke mmoja katika jimbo la Utah nchini Marekani ambaye
amechapisha kitabu cha watoto kuhusiana na machungu ya kifo cha ghafla cha
mumewe amefunguliwa mashtaka ya mauaji.
Mwanamke huyo Kouri Richins, mama wa watoto watatu, aliwaita
polisi usiku wa manane Machi 2022 na kusema mumewe Eric Richins mwili wake ni
wa baridi.
Mwanamke huyo alizieleza mamlaka kwamba alimuandalia mumewe
mchanganyiko wa kinywaji aina ya vodka, na kumkuta hana uhai saa nne baadae.
Uchunguzi wa kitabibu baadae uling’amua kwamba marehemu Eric
kifo chake kilisababishwa na kuzidisha dozi ya dawa kali ya maumivu aina ya fentanyl.
Bi. Kouri alipata dawa za fentanyl na kisha kuwa
anamchanganyia mumewe kwa lengo la kumuua, ambapo rafiki mmoja wa Eric alidai
marehemu alimueleza anahisi mkewe anamuwekea sumu.
0 Maoni