Jacob Wekesa ‘mtume’ anayetibu ugumba atiwa hatiani kwa ubakaji

 


Jacob Wekesa, anayejiita mtume, ameingia matatani baada ya kufikishwa Mahakamani Kenya kwa mashtaka ya kuwabaka mabinti wawili wa muumini wake aliyemkaribisha nyumbani kwake ‘mtume’ huyo na kukaa naye.

Wekesa wa kanisa la Legion of Mary, alikaribishwa kwa muumini wake Sarah Otieno huko Njoro, ambapo akiwa nyumbani kwa mwenyeji wake aliwarubuni mabinti wawili wa muumini wake na kuwabaka.

Mtume huyo feki, amekuwa akidai kuwa anauwezo wa kubaini mwanamke mwenye matatizo ya kupata ujauzito kwa kutumia macho yake yenye uwezo wa kiroho, na kumtibu ili aweze kushika mimba na kuza.

Mmoja wa watoto hao wa kike alieleza kuwa Wekesa alimuita chumbani kwake ambacho kilikuwa kinapakana na chao na kumuambia anamatatizo ya kukosa ujauzito na kisha akaanza kumtomasa na kisha kumbaka na kumuonya asipige mayowe.

Baada ya kumfanyia kitendo hicho, alimuambia avae nguo zake kwani amesha pona na kumuonya kuwa asimwambie mtu yeyoye, kwani kunawatu wengi amewafanyia hivyo na wamekaa kimya na wamepona tatizo lao.

Hata hivyo Binti huyo hakukaa kimya alimueleza dada yake cha kushangaza dada naye aliangua kilio na kusema ‘mtume’ huyo pia amembaka na yeye kwa njia hiyo hiyo, ndipo walipoenda hospitali na daktari kuthibitisha kuwa wamefanyiwa ukatili wa kingono na kuwapatiwa dawa.

Katika utetezi wake Wekesa alidai kuwa asingeweza kuwabaka mabinti hao kwa kuwa walikuwa wanaondoka nyumbani alfajiri na kurudi usiku wa manane, na kuongeza kuwa amebambikiziwa kesi hiyo.

Hata hivyo Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Edward Obonge amemtia hatiani Wekesa kwa kosa la ubakaji na imepanga kutoa hukumu ya kesi hiyo Juni 6, mwaka huu.

Chapisha Maoni

0 Maoni