Man City yaikaba koo Arsenal ubingwa wa EPL

Manchester City imewachachafya vinara wa ligi kuu ya England Arsenal kwa kuichabanga magoli 4-1 katika  mchezo uliochezwa kwenye dimba la Etihad katika mbio za kuwania ubingwa wa ligi kuu ya England.


Kwa sasa vinara hao wa ligi hiyo, wanakalia kuti kavu kileleni baada ya Manchester City kuwasogelea kwa tofauti ya alama mbili huku wakiwa wamecheza mechi mbili zaidi ya mabingwa hao watetezi.


Msimamo wa  EPL kwa sasa uko hivi:-

ARSENAL—Mechi 33—Alama 75

MAN CITY—Mechi 31—Alama 72

Newcastle—Mechi 31—Alama 59

Man United—Mechi 30—Alama 59

Mchezaji Kevin De Bruyne amefunga magoli 8 dhidi ya Arsenal kwenye ligi kuu England ambapo jana alifunga magoli mawili kwenye dakika ya 6 na 53 ya mchezo wengine waliofunga ni Stone 45+1' Haaland dk 90+5 na Holding dk 86.



Arsenal ya Mikel Arteta, ilishinda taji hilo mara ya mwisho mnamo 2003-04, chini ya kocha Arsene Wenger.Wakiwinda taji la tano la Premier League ndani ya miaka sita, City pia wako kwenye kinyang’anyiro cha kuwania kombe la FA na Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Chapisha Maoni

0 Maoni