Picha za mjongeo za maandamano ni za zamani- Polisi

 

Jeshi la Polisi limeuarifu umma wa Watanzania kuwa, kuna hii picha mjongeo ya zamani na nyinginezo zinasambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikihadaa wananchi kuwa maandamano yameshaanza.

Taarifa iliyotolewa leo na Msemaji wa Jeshi la Polisi imesema hakuna jambo kama hilo kwani vyombo vya ulinzi na usalama vipo mitaani kudhibiti hali kama hiyo kama kuna ambao watakaidi kuelewa katazo lililotolewa Desemba 5,2025 kwa mujibu wa sheria za nchi.

Jeshi la Polisi Tanzania limendelea kusisitiza kuwa, kinachohamasishwa na kuitwa maandamano ya amani yasiyo na kikomo, kimepigwa marufuku kwa sababu hayajafuata na wala hayaja kidhi matakwa ya Sheria Mama ambayo ni Katiba ya Mwaka 1977 pamoja na Sheria ya Polisi na Polisi Wasaidizi Sura 322.

Chapisha Maoni

0 Maoni