Jeshi la Polisi limeuarifu umma wa Watanzania kuwa,
kuna hii picha mjongeo ya zamani na nyinginezo zinasambazwa kwenye mitandao ya
kijamii zikihadaa wananchi kuwa maandamano yameshaanza.
Taarifa iliyotolewa leo na Msemaji wa Jeshi la
Polisi imesema hakuna jambo kama hilo kwani vyombo vya ulinzi na usalama vipo
mitaani kudhibiti hali kama hiyo kama kuna ambao watakaidi kuelewa katazo
lililotolewa Desemba 5,2025 kwa mujibu wa sheria za nchi.
Jeshi la Polisi Tanzania limendelea kusisitiza kuwa,
kinachohamasishwa na kuitwa maandamano ya amani yasiyo na kikomo, kimepigwa
marufuku kwa sababu hayajafuata na wala hayaja kidhi matakwa ya Sheria Mama
ambayo ni Katiba ya Mwaka 1977 pamoja na Sheria ya Polisi na Polisi Wasaidizi
Sura 322.

0 Maoni