Utulivu wa siasa ndiyo ngao Kuu: Watanzania waaswa kutambua thamani ya nchi yao

 

Wito mzito umetolewa kwa kila Mtanzania kutafakari kwa kina na kutambua thamani halisi ya Taifa lao (Utaifa). Wataalamu wa masuala ya jamii na viongozi wa kitaifa wanasisitiza kuwa, Watanzania watakapoelewa kwa dhati uzuri na faida ya nchi yao, watailinda kwa gharama zote, hasa kwa kudumisha utulivu wa siasa.

Siraji Ali Likwati, akizungumza kwa uchungu kuhusu athari za vurugu, alikumbusha: "Tanzania yetu ni Tanzania yenye uhuru. Nchi za jirani zinatusifia kwa uhuru na mshikamano." Hii ndiyo sifa ambayo inapaswa kutambuliwa na kulindwa kama hazina ya Taifa.

Utulivu wa kisiasa unaonekana wazi kuwa ndiyo msingi wa maisha ya kila Mtanzania. Pale utulivu unapopotea, kama ilivyoonekana kwenye kauli za wananchi:

Faizat Peter alikiri kwamba, bila amani, "Maisha ya Mtanzania asilimia kubwa ni utoke ili upate kuishi" huwa magumu sana.

Habib Sadick alisisitiza kuwa hata kama mtu ana fedha, hawezi kuzifanyia chochote "kwa kuwa kipindi kile hakina amani kidogo."

Mchambuzi mmoja wa Siasa za Ndani anasema: "Siasa tulivu huruhusu uchumi kukua, huduma za jamii kufanya kazi, na wananchi kupanga maisha yao bila hofu. Pale wanasiasa wanapogombana, ni raia wa kawaida ndiye anayelipa gharama kwa njaa na ukosefu wa usalama."

Utaifa wa kweli unahusisha kuweka maslahi ya Taifa mbele kuliko yale ya mtu binafsi au kikundi hata Maandiko matakatifu ya Biblia na Qur'an yanafundisha umuhimu wa heshima kwa mamlaka na utulivu. Utambuzi wa thamani ya Taifa letu ni jukumu la kimaadili na kiroho. Tuache tamaa zinazoweza kutuvuruga.

Tunapaswa kurejea kwenye mafundisho ya Mababa wa Taifa, ambao walijenga nchi hii kwa misingi ya Umoja na Amani, licha ya utofauti wetu. Kila Mtanzania anahimizwa kuangalia zaidi kwenye yale yanayotuunganisha, na kutumia Mashauriano na Upendo kutatua tofauti zozote zinazojitokeza kisiasa.

Kila Mtanzania, kuanzia vijana kama Salma Juma Kimaro aliyesisitiza kuwa tusifanye mambo ya kuiga, hadi viongozi wa dini na siasa, anapaswa kubeba jukumu la kulinda mhimili huu mkuu.

Utambuzi wa thamani ya Taifa letu unatuagiza kudumisha Utulivu wa Siasa kwa gharama zote. Tukijua thamani ya amani, tutaona kwamba hakuna malengo ya kisiasa yanayostahili kupoteza maisha au kusababisha njaa kwa wananchi. Amani ya sasa ndiyo dhamana ya Taifa la kesho.Imeelezwa kuwa Watanzania watakapojua thamani ya nchi yetu, watailinda kwa gharama zote, hasa kwa kudumisha utulivu wa siasa.

Siraji Ali Likwati anasema, "Tanzania yetu ni Tanzania yenye uhuru. Nchi za jirani zinatusifia kwa uhuru na mshikamano." Utaifa unajengwa kwa kuweka maslahi ya taifa mbele kuliko yale ya mtu binafsi au kikundi.

 "Utulivu wa kisiasa ndiyo msingi wa uwekezaji. Pale amani inapopotea, wawekezaji huondoka, na maendeleo husimama. Utaifa wa kweli ni kuhakikisha tunaacha urithi wa amani kwa vizazi vijavyo."

Tunahimizwa kuchukua jukumu, kutumia Mashauriano badala ya Vurugu, na kuimarisha Uzuri wa Maadili yetu ili kujenga Tanzania yenye ustawi na amani ya kudumu.



Chapisha Maoni

0 Maoni