Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, amevielekeza vyombo
vya sheria hasa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka kuona uwezekano kuwafutia
mashtaka vijana waliohusika kwa kufuata mkumbo katika vurugu za uchaguzi mkuu
Oktoba 29, mwaka huu.
Rais Dkt.
Samia ametoa msamaha huo leo Jijini Dodoma katika hotuba yake ya ufunguzi wa
Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kusema kuwa kuna wakati
vijana hufuata mkumbo wa uhalifu kwa ushabiki na kuna vijana wengi waliokamatwa
hawakujua wanachofanya ni uhaini.
Rais Dkt.
Samia amemuelekeza Mkurugenzi wa Mashtaka kuangalia kwa wale vijana ambao
wamefuata mkumbo na hawakudhamiria kufanya uhalifu awafutie makosa yao.
Aidha, Rais
Dkt. Samia ametoa wito kwa vijana wa Tanzania, kwa kuwaeleza kuwa nchi hii
imejengwa kwa amani na utulivu wa kisiasa, na kuongeza kuwa endapo wazazi wao
wangeshawishika kama walivyofanya wao nchi isingekuwa na neema na
maendeleo wanayoyaona.

0 Maoni