Uchaguzi huo!!: Ajira hizi si geresha, ni utekelezaji wa ahadi za kazi na utu kwa kizazi chetu!

 

Wakati dunia inashuhudia ongezeko la maandamano na migomo ya vijana waliokata tamaa kutokana na ukosefu wa ajira, Serikali ya Awamu ya Sita imeandika ukurasa mpya wa matumaini kwa kutangaza zaidi ya nafasi 40,000 za ajira katika sekta mbalimbali.

Tukielekea Uchaguzi Mkuu, ni muhimu kutambua kwamba ajira hizi si "geresha" (za kuwavutia wapiga kura), bali ni mwendelezo halisi wa utekelezaji wa ahadi mbalimbali za Serikali kwa wananchi wake, zikisimamia misingi ya Kazi na Utu.

Wakati mataifa mengine yakikabiliwa na janga la ukosefu wa ajira kama vile Afrika Kusini yenye zaidi ya 43% au Ulaya zaidi ya 25% Tanzania inaendelea kujenga matumaini kwa kuongeza bajeti ya ajira katika Mwaka wa Fedha 2025/26. Huu ni ushahidi wa dhati wa Serikali kuleta fursa na ustawi kwa vijana.

 UPOTOSHAJI WA MITANDAONI

Tunasikitishwa na kauli za kukatisha tamaa kutoka kwa watu wachache kwenye mitandao ya kijamii wanaodai ajira hizi ni "geresha." Ukweli ni mmoja: Ajira hizi ni halisi, zimetangazwa rasmi kupitia Ajira Portal, na tayari maelfu ya Watanzania wameitwa kwenye usaili. Kauli kama hizi si tu zinaua matumaini ya vijana, bali pia zinavuruga ari ya Taifa.

Ajira ni Neema, Si Hadithi za Mitandaoni: Hadithi ya Damas Mhagama, aliyeajiriwa baada ya uthubutu na uvumilivu licha ya changamoto za kiufundi, inathibitisha kuwa mafanikio hayaji kwa malalamiko bali kwa kuchukua hatua.

Chagua Kazi Badala ya Maneno: Kila tangazo la kazi ni mwaliko wa kubadili maisha yako. Tumia kifurushi chako cha intaneti kutafuta taarifa za ajira, mafunzo, na fursa za ujasiriamali, badala ya kusambaza upotoshaji na vichekesho visivyo na tija.

Ajira ni zaidi ya kipato; ni jukwaa la kujijenga, kujitegemea, na kujenga Taifa lenye uchumi wa kizalendo ambalo linabakia salama na tulivu ili kuendeleza maendeleo haya.

Chapisha Maoni

0 Maoni