Rais Samia aidhinisha Oktoba 29 Mapunziko, Watu wakatiki

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameidhinisha Oktoba  29, 2025 kuwa siku ya mapumziko ili kuwawezesha Wananchi kupiga kura, kwa kutumia mamlaka aliyonayo chini ya Sheria ya Sikukuu za Kitaifa sura ya 35, taarifa iliyotolewa leo na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka imesema.

“Kama inavyofahamika, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza siku ya Jumatano tarehe 29 Oktoba, 2025 kuwa siku ya kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa mwaka 2025,” imesema taarifa hiyo na kuongeza “uamuzi huo wa Rais umekuja kwa madhumuni ya kuwawezesha Wananchi wenye sifa stahiki wakiwemo Watumishi wa Umma na Wafanyakazi katika Sekta Binafsi kutumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura,” imeeleza taarifa hiyo.



Chapisha Maoni

0 Maoni