Puuzeni ndoto ya machafuko za ‘Mchumia tumbo’

 

Mange Kimambi, mfanyabiashara wa mitandao anayeishi Marekani, kazi yake kuu ni kuchochea fujo ili apate content (naudhui) ya kuuzia wafuasi wake na kujikusanyia mabilioni ya shilingi. Ndoto yake ya kuona vurugu na fujo zikilipuka Tanzania inabaki kuwa biashara ya kutengeneza maudhui ya uongo na kuzua mtafaruku.

Wiki hii, Mange ameonekana tena akitoa maelekezo kwa vijana na wanajeshi wa Tanzania kuhusu mpango wake wa kuichafua nchi. Hata hivyo, mara hii, sauti yake ilikuwa ilijaa shaka, akionesha woga wa kutofanikiwa kwa mpango huo wa kibiashara.

Ukweli wa Biashara Yake:

Mange anafanya biashara ya maudhui yenye misingi ya chuki, matusi, na fedheha dhidi ya viongozi, wasanii, na wanasiasa. Biashara hii inamuingizia zaidi ya Shilingi Bilioni 1.5 kwa mwezi, huku kila subscriber akilipa takribani Shilingi 1,500. Huu ndio msingi wa uchochezi wake, si ajenda ya kizalendo.

Vijana Waendelee Kumpuuza:

Maandamano aliyoyapanga Marekani, katika Ubalozi wa Tanzania Washington DC, yalihudhuriwa na watu wasiozidi kumi. Hii ilithibitisha kwamba vijana wa Tanzania wamepuuza na kutambua udanganyifu wake. Licha ya Watanzania zaidi ya 100,000 kuishi Marekani, hakuweza kukusanya hata asilimia ndogo sana!

Uoga wa 'Mwanaharakati': Mange mwenyewe hakuthubutu kujitokeza, akidai jeshi la Marekani limemwonya. Je, huu ndiyo ujasiri wa kiongozi anayedai anaongoza kizazi cha mabadiliko? Vijana, mpuzeni kiongozi mwenye woga anayetaka kuwahatarisha wengine.

Tanzania Ni Nchi Ya Kazi, Siyo Ya Kelele: Wakati Mange anataka machafuko, vijana wa Tanzania wako kazini, wanasomea taaluma, wanabuni biashara, na kushiriki katika shughuli za maendeleo ikiwamo kilimo na utalii. Katika kilimo mashamba ya umwagiliaji yameongezeka kutoka hekta 540,000 (2021) hadi zaidi ya milioni moja (2024).

Pia pato la taifa kutoka utalii limeongezeka, na vijana wako Zanzibar, Arusha, na Kilimanjaro wakihudumia watalii zaidi ya Milioni 5.3!

Tanzania ni Taifa lenye amani, matumaini, na kazi. Uchochezi wa Mange Kimambi utabaki hewani kama matangazo ya mtandaoni yasiyo na tija. Vijana, endeleeni kulinda amani, fanyeni kazi, na msimpe "content" ya fujo anayoitaka.

Chapisha Maoni

0 Maoni