Sito muacha Majaliwa kwenye Serikali yangu - Mwalimu

 

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Salim Mwalimu amesema kwamba hatomuacha Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa iwapo atachaguliwa kuwa rais katika uchaguzi mkuu Oktoba 2025.

Malimu ametoa kauli hiyo jana akiwa mkoani Lindi, katika mwendelezo wa kampeni za chama hicho, ambapo ameahidi kutoaacha uzoefu wa miaka 10 ya Uwaziri Mkuu wa Mhe. Majaliwa upotee hivi hivi.

“Mimi nawaahidi kuwa sitamuaacha Mhe. Majaliwa katika serikali yangu nitakayoiunda mtakapo nichagua, nitafanya kazi na majali atapata nafasi yake ili aendelee kutupatia uzoefu wake,” alisema Mwalimu.

Amesema kwamba yeye hatoingia Ikulu kufukua makaburi, wala hana mpango wa kuwahukumu watu bali atafanya maridhiano ya kitaifa na kuwasamehe wale wote waliofanya makosa wakiwa madarakani.

“Nawaahidi serikali yangu kamwe haitaenda kulipa kisasi wala kumuhukumu mtu, sisi sote ni wanadamu na mwanadamu ameumba wakiwa na uwezo wa kufanya makosa, hivyo mimi si Mungu niwahukumu,” alisema Mwalimu.

Amesema kwamba hata Jeshi la Polisi hatofanya mabadiliko ataendelea na hao hao akiwamo Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Camillius Wambura, “Nitaendelea na IGP Wambura simfukuzi kazi labda ajitekenye mwenywe (akosee) mimi nifanyaje sasa ?,” alisema Mwalimu.

Chapisha Maoni

0 Maoni