Aliyekuwa
Waziri Mkuu wa Kenya na Kiongozi wa Chama cha Orange Democratic Movement (ODM),
Bw. Raila Amolo Odinga, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 80.
Kifo
chake kilithibitishwa leo na Rais wa Kenya, Dkt. William Ruto pamoja na familia
ya marehemu, wakieleza kuwa Bw. Odinga alikuwa akipatiwa matibabu katika
hospitali moja nchini India.
Taarifa
za msiba huu zimekuja huku kukiwa na uvumi uliozuka mapema wiki hii, uliodai
kuwa mwanasiasa huyo mkongwe alikuwa katika hali mahututi.
Hata
hivyo, familia yake ilikuwa imejitokeza mapema na kuwahakikishia Wakenya kuwa
hali yake ilikuwa thabiti na alikuwa akiendelea vyema na matibabu.
Seneta wa
Kaunti ya Siaya na kaka mkubwa wa marehemu, Dkt. Oburu Odinga, aliwatoa hofu
Wakenya kwa kusema kuwa Bw. Odinga alikuwa katika hali nzuri na alikuwa akipata
nafuu nchini India baada ya kuugua ghafla.
Marehemu
Raila Odinga atakumbukwa kama mmoja wa wanasiasa mashuhuri na wenye ushawishi
mkubwa katika historia ya Kenya, ambaye alihudumu katika nyadhifa mbalimbali za
kisiasa na kushiriki pakubwa katika harakati za mageuzi ya kisiasa nchini humo.

0 Maoni