Asilimia
82 ya wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wanaingia kwenye ajira
moja kwa moja baada ya kuanzishwa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi
(HEET) mwaka 2021.
Kauli
hiyo imetolewa jana na Makamu Mkuu wa UDSM, Prof. Wiilliam Anangisye katika
semina ya siku moja na wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam
kuhusu mafanikio ya mradi huo.
“Miongoni
mwa mafanikio ya HEET ni kwamba, haupiti mwaka mmoja zaidi ya asilimia 82 ya
wahitimu wanaingia kwenye ajira,” amesema.
Amesema,
mradi huo umewezesha wanafunzi wa chuo hicho kuhitimu wakiwa wameiva kwa ujuzi
jambo ambalo ndio hitajio kubwa la soko la ajira kwa sasa.
Naibu
Mratibu wa HEET, Prof. Liberato Haule amesema, mradi huo umefanikisha kujenga
jumla ya majengo 21 katika Mikoa ya Lindi, Kagera, Dar es Salaam na visiwani
Zanzibar ili wanaohitaji chuo hicho, waweze kusoma wakiwa katika maeneo hayo.
“Ujenzi
wa miundombinu hii umefika asilimia 65. Mradi huu (HEET) kwa ujumla
umetekelezwa kwa asilimia 80,” amesema.
Baada ya
ziara fupi kwenye baadhi ya majengo mapya ya Mradi wa HEET, Mwenyekiti wa
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile amesema, UDSM imeondokana na
unyumbani kwa kutanua elimu kwenye mikoa iliyojenga majengo yake.
“Hili ni
jambo zuri sana, tusimame na mazuri yanayofanywa na nchi, tusipofanya sisi
hakuna ambaye atakuja kutusemea,” amesema.
Mradi wa
HEET unaotekelezwa kwa miaka mitano (2021 - 2026), umelenga kuimarisha elimu ya
juu nchini kwa kuwekeza miundombinu, kuboresha mitaala na kuimarisha
ushirikiano kati ya Vyuo Vikuu na Sekta Binafsi ambapo kiasi cha Dola za
Marekani Milioni 47.5 zilitengwa kwa ajili ya mradi huo.
Mpaka
sasa jumla ya mitaala 250 tayari imeithinishwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

0 Maoni