Mpinzani Venezuela ashinda Tuzo ya Amani ya Nobel

 

Kiongozi wa upinzani nchini Venezuela, María Corina Machado, ametangazwa kuwa mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel kwa mwaka huu, kutokana na juhudi zake zisizochoka katika kupigania haki za kidemokrasia kwa wananchi wa taifa hilo la Amerika Kusini.

Machado, ambaye amekuwa akiishi mafichoni tangu uchaguzi wa urais uliofanyika mwaka jana, ametambuliwa kwa "kazi yake ya kuhamasisha mabadiliko ya haki na yenye amani kutoka utawala wa kiimla kuelekea demokrasia".

Kamati ya Nobel imeeleza kuwa Machado ni "mmoja wa mifano ya kipekee ya ujasiri wa kiraia katika Amerika Kusini katika nyakati za hivi karibuni."

Tangu aanze harakati zake za kisiasa, Machado amekuwa mstari wa mbele kupinga utawala wa sasa nchini Venezuela, akitaka mageuzi ya msingi yanayowapa wananchi nafasi ya kuchagua viongozi wao kwa njia huru na ya haki.

Chapisha Maoni

0 Maoni