Kauli ya Zitto Kabwe kwenda kuleta mabadiliko kupitia Sanduku la Kura yaungwa mkono!

 

Kumekuwa na maoni tofauti Mtandaoni, mengi yakiunga mkono kauli ya  mmoja wa viongozi wa upinzani Zitto Kabwe ya kuwataka Watanzania kupuuza wanaotoa wito wa kutopiga kura Oktoba 29.

Katika klipu ya moja ya hotuba zake katika kampeni akiwa Songea, Zitto anatoa wito wa wananchi kuwafikiria wanaohimiza kutopiga kura kama watu wenye walakini ingawa wengine anawaheshimu.

 Zitto Kabwe  anayetokea ACT Wazalendo na mgombea ubunge Kigoma, alisisitiza watu kutoka kwenda kupiga kura kwani kutofanya hivyo ni kama kununuliwa na chama tawala kukiacha kifanye kinavyotaka.

Zitto anasema watu wanaohimiza wengine wasishiriki katika kupiga kura wana walakini vichwani mwao kutokana na umuhimu wa zoezi hili.

Kauli ya Zitto inachagiza ukweli kuwa kura si tu haki, bali ni mamlaka ya kuajiri viongozi wa nchi. Kauli ya Zitto imelenga kuwaamsha Watanzania wachanga kutokubali kupuuzia mchakato huu.

Umuhimu wa uchaguzi unasisitizwa kwa data za vitendo kwani taifa linatakiwa kuendelea kusonga mbele kijamii na kiuchumi kutoka katika msingi uliowekwa.

Serikali  ya sasa imewekeza mabilioni ya shilingi katika miundombinu ya kisasa kama vile Mabasi ya Mwendokasi (BRT), ujenzi wa Hospitali mpya 50 za wilaya, na upanuzi wa vituo vya afya.

Kwenda kupiga kura Oktoba 29 ni fursa ya kuajiri Msimamizi: Kura inakupa wewe uwezo wa kuhoji na kuchagua viongozi watakaoweza kulinda na kusimamia urithi huu wa Taifa, na kuhakikisha huduma bora za afya, elimu, na usafiri zinasonga mbele.

Aidha ni fursa ya Kudai Uwajibikaji: Vijana wanahimizwa kuhoji wagombea kwa kutumia sanduku la kura kuhusu changamoto mbalimbali zinazowakabili wakiwa miongoni mwa wanajamii.

Matusi na uharibifu wa mali za umma (kama vile mabasi ya BRT na vizimamoto) hauna nafasi katika siasa ya karne ya 21. Kura yako ni ya ustaarabu na ndiyo njia pekee ya kulinda urithi wa Taifa.


Chapisha Maoni

0 Maoni