Joe Biden, apatiwa tiba ya mionzi ya saratani ya tezi dume

 

Aliyekuwa Rais wa Marekani, Joe Biden, ameanza kupatiwa matibabu ya mionzi (radiation therapy) kama sehemu ya tiba yake dhidi ya saratani ya tezi dume, msemaji wake amethibitisha.

Kwa mujibu wa msemaji huyo, Biden mwenye umri wa miaka 82 pia anapatiwa matibabu ya homoni, ingawa hakufafanua zaidi kuhusu hatua hiyo ya matibabu.

Taarifa kutoka kwa chanzo kilichoelezwa na shirika la habari la NBC News zinaeleza kuwa matibabu ya mionzi yanatarajiwa kuchukua kipindi cha wiki tano, hali inayochukuliwa kama hatua mpya katika safari yake ya kiafya.

Biden aliondoka madarakani mwezi Januari akiwa Rais mzee zaidi kuwahi kuhudumu katika historia ya Marekani, na hali ya afya yake iliibua maswali mengi wakati wa muhula wake wa kwanza.

Maswali hayo yalimfanya hatimaye kuamua kujiondoa katika kinyang’anyiro cha kuwania urais kwa muhula wa pili, akiwa tayari ameanza kampeni za kuchukua tena nafasi hiyo.

Chapisha Maoni

0 Maoni