Katika
ziara ya Uhamasishaji wa Matumizi sahihi ya Mbolea Kanda ya Nyanda za Juu
Kusini, inayoongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Dkt. Steven
Nindi, uongozi wa Wilaya ya Chunya umeomba wataalam wa Kilimo kuongeza wigo wa
kutoa elimu ya Matumizi sahihi ya Mbolea kwani Kilimo ni sayansi na matumizi ya
Mbolea yanahitaji vipimo sahihi kulingana na afya ya udongo.
Rai hiyo
imetolewa leo tarehe 04.10.2025 katika kikao kilichofanyika katika ofisi ya
Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mkoani Mbeya ambapo Mkuu wa Wilaya ya Chunya SACI
Mbaraka Batenga ameeleza kuwa upimaji wa afya ya udongo ni muhimu unamwezesha
mkulima kuwa na utaalam, kutumia mbolea kwa usahihi na kuongeza uzalishaji wa
mazao.
“Msimu wa
Kilimo ulioisha mwaka 2024/2025, zao la tumbaku limefanya vizuri, mbolea
iliyosambazwa na TFC imeongeza uzalishaji zaidi ya makadirio yaliyokuwepo
ambapo Wilaya ya Chunya imezalisha tani milion 27,091.7 na kuondoa malalamiko
kwa wakulima,” ameeleza SACI Batenga.
Pamoja na
mafanikio hayo ameeleza kuwa bado yapo maeneo ambayo hayana mwamko wa kutumia
mbolea kama eneo la kata ya Kambi Katoto na Sipa hivyo endapo watapewa elimu ya
matumizi ya Mbolea watahamasika kutumia mbolea na kuongeza uzalishaji.
Kwa
upande wake Dkt. Stephen Nindi amepongeza juhudi za viongozi kuhakikisha
wanapata mashine za kupimia afya ya udongo ili kumrahisishia mkulima kutambua
aina ya udongo na mbolea inayopaswa kutumika.
Mkurugenzi
Mkuu wa Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) Ndg. Samuel Mshote ameeleza kuwa
katika msimu wa Kilimo uliopita TFC ilisambaza tani 61,000 ya Mbolea ya NPK
10:18:24 kwa wakulima wa zao la tumbaku na kwa mwaka huu wa TFC itasambaza
takribani tani 71,000 za mbolea ya NPK 10:18:24 inaendelea kusambazwa kwa
wakulima kupitia vyama vyao vya ushirika.
Aidha,
Ndg. Mshote ameeleza kuwa hadi sasa usambazaji wa mbolea ya NPK 10:1824 kwa
Wilaya ya Chunya umefikia asilimia 85, tani 10,395 zimewafikia wakulima kati ya
tani 12,230 zinazotarajiwa kusambazwa katika msimu huu. Na kwa mbolea ya UREA
na CAN tayari zipo Nchini na zitaanza kusambazwa kWa wakulima ndani ya mwezi
huu wa Oktoba, 2025.
0 Maoni