CHADEMA: Kuvunja sheria makusudi si mkakati wa kisiasa, ni kufilisika kwa hoja

 

Tanzania imejengwa juu ya misingi ya Sheria, utawala bora, na siasa za hoja. Hata hivyo, mwenendo unaoendelea ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) unadhihirisha dalili za chama kilichopoteza dira, kikigeuza uvunjaji wa Sheria kuwa "mkakati" wa kujitafutia huruma ya kisiasa.

Kile kilichokuwa chama chenye 'Think-Tank' imara na hoja za kitaalamu, sasa kinaonekana kuishiwa ubunifu. Badala ya kuja na mikakati ya kiufundi na kisera, tunashuhudia mbinu za kutengeneza "kiki" mitandaoni:

Kuvunja Sheria Makusudi:

Wafuasi wanavuka mipaka bila vibali, wanafanya vitendo vya kihuni, au kuanzisha vurugu nje ya Mahakama, kisha wakikamatwa, wanageuza tukio kuwa propaganda za "tumeonewa."

Kisa cha Kuhuzunisha:

Kisa cha hivi karibuni cha mwanachama wa Chadema kumvamia askari nje ya Mahakama Kuu ni mfano wa wazi wa siasa iliyofilisika; inajaribu kutengeneza "huruma" badala ya kutoa hoja.

UKWELI NI HUU:

Uongozi wa kisiasa si kinga dhidi ya Sheria. Sheria haipendelei chama, haina rangi ya bendera, ni msumeno unaokata kote. Mwanasiasa anayevunja Sheria ana wajibu wa kuwajibika kama raia mwingine yeyote.

Kujenga hadithi ya "tunadhulumiwa" kila mara siyo siasa, bali ni kuhalalisha utovu wa nidhamu na uvunjaji wa Sheria makusudi. Siasa za hoja zinahitaji maarifa, si matusi. Zinahitaji mikakati, si misemo ya huruma.

Kuvunja Sheria makusudi ili ukamatwe ni ujanja wa muda mfupi unaodhihirisha kuishiwa kimkakati, si siasa ya maendeleo, bali ni vioja vya kukosa dira.

Tanzania inahitaji upinzani makini unaotoa hoja zenye mashiko.Turejee kwenye misingi ya uwajibikaji na nidhamu ya kisiasa.

Chapisha Maoni

0 Maoni