Wananchi
wapatao 814 wamehudumiwa kwenye banda la Wakala ya Barabara za Vijijini na
Mijini (TARURA) katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Madini yaliyomalizika
mwishoni mwa wiki mkoani Geita.
Afisa
Ustawi wa Jamii kutoka TARURA mkoa wa Geita, Bw. Godfrey Vedasto amesema
wananchi hao walifika katika banda la Wakala huo kupata elimu kwa ujumla ya
namna wanavyotekeleza majukumu yao lakini pia kupata uelewa wa namna
wanavyoshughulikia utatuzi wa ubovu wa barabara katika maeneo yao.
“Jumla ya
wananchi 814 walitembelea banda letu, wanaume 444 na wanawake 374, wengi
walitupongeza kwa kazi kubwa tunayoifanya ya kufungua barabara katika maeneo
yao, pia wengine walitaka kufahamu namna tunavyoweza kutatua changamoto za
ubovu wa barabara katika maeneo yao.”
Amesema
pia wananchi walitaka kupata uelewa kuhusu fidia katika miradi inayokusudiwa
kutekelezwa na Wakala huo.
“Ipo
miradi ambayo wananchi hulipwa fidia, sisi kama TARURA huwa tunatoa elimu kabla
ya mradi kutekelezwa, sema wapo baadhi ya wananchi bado wanahitaji elimu zaidi”,
ameongeza kusema.
Hata
hivyo, amesema elimu ya utunzaji wa miundombinu ya barabara ilitolewa na
kuwakumbusha wananchi waendelee kuwa mabalozi wazuri wa kulinda barabara pamoja
na mitaro ya maji ili idumu muda kwa mrefu.
Amemaliza
kwa kusema kwamba maonesho hayo kwa TARURA yamekuwa na tija kubwa kwani
wameweza kuwafikia wananchi wengi na kutatua changamoto zao
katika maeneo yao.


0 Maoni